Wednesday, May 15, 2019

WhatsApp: Fahamu namna ya kuwa salama unapotumia mitandao ya kijamii

SHARE

whatsapp logo

Taarifa kwamba "WhatsApp inaweza kudukuliwa" sio jambo ambalo mtumiaji yoyote wa mtandao huo wa kijamii anataka kusikia wala kuona katika kichwa cha habari.
Alafu kuongezea kwamba "Wadukuzi walifanikiwa kuweka mfumo wa uangalizi" na kitengo cha habari cha kampuni hiyo wana kibarua kikubwa mikononi mwao.
WhatsApp linasema akaunti kadhaa zililengwa na " mdukuzi mkuu wa mitandao".

Lakini iwapo kauli hii imekutia wasiwasi, haya ni baadhi ya mambo unayostahili kufanya kuhakikisha mawasiliano yako yapo salama.

Udukuzi huo uligunduliwa kwanza mapema mwezi huu.
Wakati huo Facebook, inayomiliki mtandao wa WhatsApp, iliwaambia maafisa wa usalama kwamba lilikuwa : "pengo katika mawasiliano ya sauti ya WhatsApp VOIP [voice over internet protocol] iliyoruhusu udukuzi kupitia vifurushi vya mfumo wa SRTCP [secure real-time transport protocol] vilivyotumwa kwa nambari ya simu ya mlengwa."

Hata kama simu haikushikwa, mfumo huo wa udukuzi uliidhinishwa kutokana na pengo hilo katika mawasiliano ya sauti ambao hauna usalama wa kutosha.
Simu pengine ilikatika na haionekani kwenye orodha ya waliopiga simu katika simu yenyewe, kwasababu wadukuzi walikuwa tayari wameidhibiti.

messaging logos


kulinda usalama wa taarifa zako whatsapp fanya yafuatayo!!!
  1. nenda katika whatsapp setting
  2. bofya account .
  3. bofya tena two step verification
  4. bofya tena enable
  5. weka PIN/namba za siri
  6. bofya tena change email adress ,weka email
  7. bofya tena confirm email
  8. mwisho bofya done. utakuwa umemaliza!!!


Usihifadhi taarifa zako kwenye anga la mtandao

cyber attack
Licha ya kwamba mawasiliano yanalindwa katika WhatsApp, epuka kuhifadhi taarifa zako kwenye anga la mtandao kama Google Drive au iCloud, hapo kuna tatizo.
Anga hilo la mtandao halina usalama kwahivyo mtu yoyote anaweza kuingia na kuyafikia mawaslinao yako yote.


Iwapo unajali faragha, basi hilo ni jambo ambalo unapaswa kufikiria kuacha kulifanya.
Huenda ukapata ujumbe kwamba hifadhi mawasiliano yako - lakini iwapo unataka kulibadili hilo hivi sasa nenda kwenye eneo la kuhifadhi chati zako yaani Chat Backup, katika eneo la mpangilio wa simu yako - settings.

Programu saidizi za kuimarisha ulinzi

cyber attack

Kuna programu saidizi za kuimarisha ulinzi, uthibitisho wa mara mbili (2FA) kabla kuingia kwenye mtandao huo ambao ni njia nzuri ya kuweka data yako salama.
Ni kama wingu la ziada la usalama kuhakikisha watu wanaojaribu kuingia katika akaunti ya mtandao ni watu asili wanaosemakuwa ni wao.

Kwanza, mteja ataingiza jina lake na nywila. Baada ya hapo watahitajika kutoa alama za vidole, au sauti yao au nambari maalum zitakazotumwa na programu hiyo kwenye simu yako ambazo utatumia kufungua na kuingia kwenye akaunti ya Whatsapp na nyinginezo za kijamii.
Unaweza kulibadili hilo pia kwenye upande wa mpangilio wako wa simu.


SHARE

Author: verified_user

0 Comments: