Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ameliagiza jeshi la
polisi nchini kushughulikia chama chochote cha siasa ambacho
kitakachokiuka taratibu ikiwemo kufanya mikutano ya hadhara.
Alisema kuna baadhi ya vyama vya siasa nchini vimekuwa vikikiuka
taratibu kwa kufanya mikutano ya hadhara jambo ambalo limeshapigwa
marufuku na serikali.
“Naliagiza jeshi la polisi kupitia kwa kamshna kuwashika wale wote ambao
wanakiuka taratibu wanafanya mikutano ya hadhara na kutishia amani na
utulivu wa ulipo nchini.
Hayo aliyabanisha leo wakati akisikiliza kero za wananchi mbali visiwani
Zanzibar katika kiwanja cha Komba wapya Wilaya ya Mjini Zanzibar.
Alisema huu si wakati wa Vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhala badala yake wakite katika kushughulia maendeleo ya nchi.
Alisema kufanya mikutano ya siasa na shughuli mbalimbali za siasa ni kurejesha nyuma maendeleo ya nchi.
"Mimi nataka niwambie kuwa huu si wakati wakutambulishana vyama na
kufanya mambo ya siasa wanachotakiwa mambo ambayo yatawaingizia kipato
na kuunga jitihada za marais wetu” alisema Waiziri.
"Nataka kuwambia kuwa hatutaangalia nafasi yqa mtu, wingi wa madevu
aliokuwa nao sisi tutamshughulikia endapo akikuuka taratibu na kutishia
amni ya Nchi”aliongeza kufafanua.
Katika hatua nyingine waziri Lugola alikemea vitendo vya udhalilishaji
vinavyofanya na baadhi ya maofisa wa jeshi la polisi na baadhi ya
watendaji wa serikai.
“Tunataarifa kuwa kuna baadhi ya afisa wa jeshi la polisi hufanya
vitendo vya udhalilishaji na mambo ambayo ni kinyume na utaratibu wa
kazi zao tukimbaini tutamshughulikia”alisema Waziri.
Aidha waziri aliwaomba wananchi kushirikiana na jeshi la polisi katika kufichua wahalifu katika mitaa yao.
Mapema akimkaribisha Waziri Naibu waziri wa Wizara hiyo Mhandisi Hamadi
Yusuf Masauni alisema hali ya amani na utulivu katika mkoa wa Mjini
magharib jambo ambalo linachanguia ukuwaji wa Uchumi.
Alisema kuna baadhi ya vyama vya siasa vimekuwa vikijaribu kuvyunja
amani kwa kuandaa mikutano kinyume na sheria lakini Jeshi la polisi
litahakikisha linadhibiti mikutano hiyo ili kuiendeleza kuna baadhi ya
Vyama vya siasa vimekuwa vinaanza kuharibu amani kwa kufanya mikutano
yao kinyume amani iliopo.
Aidha Akizungumzia suala la Udhalilishaji wa kijinsia Masauni alisema
bado tatizo la udhalilishaji limekuwa tatizo kutokana na baadhi ya
Wananchi kutokubali kutoa ushahidi wakati kesi zikisikilizwa sehemu
husika.
Alisema wakati umefika kwa wananchi kuthamini juhudi za serikali katika
kupambana na tatizo la Udhalilishaji wa wanawake na watoto ili
kutokomeza tatizo hilo Nchini.
Katika mkutano huo Waziri huyo alipata fursa ya kusikiliza kero
mbalimbali zinazowakabili wananchi wa mkoa wa Mjini Magharib Unguja na
kuahidi kuzitatua haraka iwezekanavyo.
Mkuno huo ni muendelezo wa ziara zake Nchini katika kusikiliza malalamiko kwa wananchi yanayohusiana na Wizara yake.
0 Comments:
Post a Comment